Up next

Tubu sasa (Official Audio)

6 Views· 01 September 2023
proshabo
proshabo
5 Subscribers
5

Haleluyaaaa x 3
Wapendwa vipi mmemsoma Hezekia ?
Bado hatuna bibilia
Alituma wajumbe kwa Israeli na Yuda, waende kula pasaka nyumbani Yelusalemu.
Pasaka ikafanywa nyumbani kwa Bwana yesu x 2
Wakafanya amari, Israeli yote ,Ikapigwa mbiu toka berry sheba mpaka dani kati,
Wakaketi kati kula karamu kati na Bwana Yesu Kati x 2

Hawakuweza kufanya ule wakati, kwasababu hawakutubu
Baada ya Karamu Kati, wakaambiwa mrudieni Mungu
Msiwe na shingo kali, kama vile baba zenu.

Uchafu kaa mbali nao, utakuponza ukose mbingu
Maovu kaa mbali nayo, yatakutupa kwenye moto
Tubu sasa, tubu sasa

Weka yako nadhiri, nafsi yako kwa Mungu
Epuka Dhambi , usije kukosa Mbingu
Fanya toba upesi, umlaki kwa Mawingu
Paza yako sauti, ukiri wako wokovu

Mpe Bwana nafasi kaa mbali na uovu, yeye ni Wokovu wetu

Usitoke ndani , usimwache Mungu, sikia sauti, acha yako maovu x 2

Sema Bwana nasi, twahitaji yako nguvu
Ulitufia msalabani, tumepata wokovu x 2

Wapendwa, tupo safarini tukairithi Mbingu pamoja na baba yetu
Wapendwa tupo safarini, tuyaache maovu tusije kukosa mbingu

Uchafu kaa mbali nao, utakuponza ukose mbingu
Maovu kaa mbali nayo, yatakutupa kwenye moto
(Tubu sasa, tubu sasa x2)

Usiku, mchana na jioni nalimwita Bwana
Kwani alisema nikimwita anapatikana
Nimechoka, kuteswa nakunyanyasika
Ibilisi kanijaza moyoni mashaka
sina mwingine, zaidi yako baba Muumba
Kwenye Mwamba imara, najenga yangu nyumba
Siteketei, siangamii sitetereki, naamini baraka zitajaa rukuki


Uchafu kaa mbali nao, utakuponza ukose mbingu
Maovu kaa mbali nayo, yatakutupa kwenye moto
(Tubu sasa, tubu sasa x2) x 2

Show more

 0 Comments sort   Sort By


Up next