ื”ื‘ื

Filamu ya Yesu - Kiswahili - The Jesus Film - Swahili - Kenya ๐Ÿ‡ฐ๐Ÿ‡ช - 1Billion.org

8 ืฆืคื™ื•ืชยท 06 ืื•ื’ื•ืกื˜ 2023
proshabo
proshabo
5 ืžื ื•ื™ื™ื
5
ื‘ Sermons

https://1billion.org/swahili/
#Filamu ya Yesu #Yesu #Kiswahili

1. Upendo
Mungu anakupenda na ana mpango kwa ajili yako.
Biblia inasema, โ€œKwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa mileleโ€ (Yohana 3:16).
Yesu alisema, โ€œmimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao teleโ€ โ€” maisha kamili yenye kusudi (Yohana 10:10).
2. Kutenganishwa
Sisi ni wenye dhambi na tumetenganishwa na Mungu.
Sote tumefanya, kufikiria au kusema mambo mabaya, ambayo Biblia huita โ€œdhambi.โ€ Biblia inasema, โ€ kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Munguโ€ (Warumi 03:23).
Mshahara wa dhambi ni mauti, utenganisho wa kiroho na Mungu (Warumi 6:23).
3. Yesu
Mungu alimtuma Yesu kufa kwa ajili ya dhambi zako.
Hii ni habari njema.
Yesu alikufa kwa ajili yetu ili tuweze kuwa na uhusiano na Mungu na kuwa pamoja Naye milele.
โ€œMungu Onyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetuโ€ (Warumi 5:8).
Lakini haikukoma alipokufa msalabani. Alifufuka tena na bado anaishi!
โ€œYesu alikufa kwa ajili ya dhambi zetuโ€ฆ Akazikwaโ€ฆ Akafufuka siku ya tatu, kulingana na Maandikoโ€ (1 Wakorintho 15:3-4).
Yesu ndiye njia ya pekee ya kumfikia Mungu
Yesu alisema:, โ€œMimi ni njia, na ukweli na uhai; hakuna mtu awezaye kuenda kwa Baba, ila kupitia kwanguโ€ (Yohana 14:6).
4. Omba
Omba ili upate msamaha wa Mungu.
Kuomba ni kuzungumza na Mungu tu. Anakujua. Kilicho muhimu ni mtazamo wa moyo na uaminifu wako. Omba sala kama hii ili umkubali Yesu kama Mwokozi wako:

โ€œYesu Kristo,
naomba msamaha kwa mambo mabaya niliyoyafanya katika maisha yangu. Asante kwa kufa Msalabani kwa ajili yangu, niweke huru kutoka kwa dhambi zangu zote na unisamehe leo. Tafadhali ingia maishani mwangu na unijaze na Roho wako Mtakatifu. Ishi nami milele.
Asante Yesu!โ€

Ulisali?

ืœื”ืจืื•ืช ื™ื•ืชืจ



ื”ื‘ื