- Sermons
- āϏāĻā§āĻā§āϤ
- Bible Teachings
- āĻā§āϞāĻžāϧā§āϞāĻž
- āĻā§āϰāĻŽāĻŖ āĻ āĻāĻāύāĻž
- āĻā§āĻŽāĻŋāĻ
- āĻŽāĻžāύā§āώ āĻāĻŦāĻ āĻŦā§āϞāĻ
- āĻāĻŽā§āĻĄāĻŋ
- āĻŦāĻŋāύā§āĻĻāύ
- āϏāĻāĻŦāĻžāĻĻ āĻ āϰāĻžāĻāύā§āϤāĻŋ
- āĻāĻŋāĻāĻžāĻŦā§ āĻāĻŦāĻ āĻļā§āϞā§
- āĻ āϞāĻžāĻāĻāύāĻ āĻāĻŦāĻ āϏāĻā§āϰāĻŋāϝāĻŧāϤāĻž
- āĻ āύā§āϝāĻžāύā§āϝ
Filamu ya Yesu - Kiswahili - The Jesus Film - Swahili - Kenya đ°đĒ - 1Billion.org
https://1billion.org/swahili/
#Filamu ya Yesu #Yesu #Kiswahili
1. Upendo
Mungu anakupenda na ana mpango kwa ajili yako.
Biblia inasema, âKwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa mileleâ (Yohana 3:16).
Yesu alisema, âmimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao teleâ â maisha kamili yenye kusudi (Yohana 10:10).
2. Kutenganishwa
Sisi ni wenye dhambi na tumetenganishwa na Mungu.
Sote tumefanya, kufikiria au kusema mambo mabaya, ambayo Biblia huita âdhambi.â Biblia inasema, â kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Munguâ (Warumi 03:23).
Mshahara wa dhambi ni mauti, utenganisho wa kiroho na Mungu (Warumi 6:23).
3. Yesu
Mungu alimtuma Yesu kufa kwa ajili ya dhambi zako.
Hii ni habari njema.
Yesu alikufa kwa ajili yetu ili tuweze kuwa na uhusiano na Mungu na kuwa pamoja Naye milele.
âMungu Onyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetuâ (Warumi 5:8).
Lakini haikukoma alipokufa msalabani. Alifufuka tena na bado anaishi!
âYesu alikufa kwa ajili ya dhambi zetuâĻ AkazikwaâĻ Akafufuka siku ya tatu, kulingana na Maandikoâ (1 Wakorintho 15:3-4).
Yesu ndiye njia ya pekee ya kumfikia Mungu
Yesu alisema:, âMimi ni njia, na ukweli na uhai; hakuna mtu awezaye kuenda kwa Baba, ila kupitia kwanguâ (Yohana 14:6).
4. Omba
Omba ili upate msamaha wa Mungu.
Kuomba ni kuzungumza na Mungu tu. Anakujua. Kilicho muhimu ni mtazamo wa moyo na uaminifu wako. Omba sala kama hii ili umkubali Yesu kama Mwokozi wako:
âYesu Kristo,
naomba msamaha kwa mambo mabaya niliyoyafanya katika maisha yangu. Asante kwa kufa Msalabani kwa ajili yangu, niweke huru kutoka kwa dhambi zangu zote na unisamehe leo. Tafadhali ingia maishani mwangu na unijaze na Roho wako Mtakatifu. Ishi nami milele.
Asante Yesu!â
Ulisali?