Up next

UTAKATIFU

2 Views· 06 August 2023
proshabo
proshabo
5 Subscribers
5

Utakatifu ni nguvu ya MUNGU inayomuwezesha mtu kuacha dhambi.

MTAZAMO WA WANADAMU
*Hakuna mtakatifu duniani
*Maisha ya utakatifu haiwezekani ukiwa duniani

MTAZAMO WA MUNGU
*Duniani wapo watakatifu
Zaburi 16:3
Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora,hao ndio niliopendezwa nao.

*Inawezekana kuwa mtakatifu ukiwa hapa hapa duniani.
Ayubu alikuwa mwanadamu kama wewe na mimi.
Ayubu 1:1
Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi,jina lake alikuwa akiitwa Ayubu;mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu,ni mmoja aliyemcha Mungu,na kuepukana na uovu.

*Watakatifu wapo duniani.Shetani asikudanganye kwamba hakuna watakatifu hapa duniani.
Hawa ni watakatifu waliokuwa wakiishi duniani kama mimi na wewe.
Mathayo 27:51-52
Na tazama pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini,nchi ikatetemeka;miamba ikapasuka.
Makaburi yakafunuka ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala.

*Mambo unayopitia siyo sababu ya kumuacha Mungu na kutenda dhambi.
Wapo waliopita pagumu zaidi yako lakini hawakumuacha Mungu.
Wewe umekosa ajira tu kwa miaka miwili unaamua kumuacha Mungu na kuanza kufanya biashara haramu,au unaanza kuiba au kulala na boss ili akupatie kazi!
Ayubu 1:22
Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi wala hakumwazia Mungu kwa upumbavu.

*Tumeitwa kuwa watakatifu.
Kama Mungu angekuwa anaona utakatifu ni kitu kisichowezekana hapa duniani asingetuita kuwa watakatifu.
1Petro 1:15-16
Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu,ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote,kwa maana imeandikwa mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

*Inawezekana kuwa watakatifu/wakamilifu ndiyo maana katuambia tuwe wakamilifu..Mungu hawezi kusema kitu ambacho anajua hakiwezekani.
Mathayo 5:48
Basi ninyi mtakuwa wakamilifu,kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.

*Utakatifu unawezekana humu humu ulimwenguni kwenye kila aina ya uovu.Kama ingekuwa haiwezekani angesema mtakuwa watakatifu kama mimi mkiishafika mbinguni.
1Yohana 4:17b
Kwa kuwa kama yeye alivyo,ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.

**Shetani anatumia mbinu hii ya kuwaaminisha watu ya kwamba haiwezekani na hakuna mtakatifu hapa duniani ili kuwateka wengi.Kwa sababu ukiishasema kwamba haiwezekani,ukiishatia akilini ya kwamba ni kitu kisichowezekana,haitawezekana na hautakuja kuishi maisha matakatifu.

**Ni kweli kwa uwezo wako wewe mwenyewe hauwezi,haiwezekani ila kwa nguvu za Mungu inawezekana.
Yesu ndiye aliyetufanya kuwa watakatifu.Lakini ni jukumu lako kukubali ukweli huu na kuamua kuiishi hii kweli.
Hakuna mtu anayeweza kuishi maisha matakatifu kwa nguvu zake,kwa akili zake,kwa ujanja wake bali ni Yesu ndiye anayetuwezesha kuishi maisha matakatifu.Ukiamua kuiishi hii kweli Mungu anaingilia kati anakusaidia.Lakini ukiitupilia mbali kweli hii hautaweza kamwe.

Show more

 0 Comments sort   Sort By


Up next